Na Mahmoud Zubeiry:
DAR ES SALAAM
YANGA SC wamepewa sharti moja tu na
Bodi ya Ligi, ambalo wakitekeleza
watapatiwa Sh. Milioni 155.
Sharti gani hilo? Msimu uliopita Yanga SC
walisusia fedha za haki ya matangazo ya
Televisheni ya Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara zinazotolewa na Azam Media
Limited kwa sababu wao walikuwa
wanapinga kampuni hiyo kupewa Mkataba
huo.
Lakini jitihada zao za kuipinga Azam Media
kurusha Ligi Kuu zilishindikana kutokana na
ukweli kwamba walitoa ofa nzuri ambayo
hakukuwa na kampuni iliyofikia hata nusu
yake.
Yanga SC wakajaribu kutaka kuzuia Azam
kurusha mechi zao, hilo nalo likashindikana
kwa kuwa ile si Ligi Kuu ya Yanga SC, ni Ligi
Kuu ya Tanzania Bara inayomilikiwa na
waliosaini Mkataba na Azam Media Limited,
TFF (Shirikisho la Soka Tanzania) na Bodi ya
Ligi.
Ilikuwa rahisi wao kujiondoa kwenye Ligi
wakacheze ligi ambayo haina Mkataba na
Azam Media, kuliko kuizuia kampuni hiyo
ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa
na familia yake kutekeleza mkataba wao na
TFF na bodi ya Ligi.
Yanga SC wakagomea fedha za mgawo wa
haki ya matangazo Sh. Milioni 100 za
msimu uliopita, ambazo Azam Media
walizikabidhi kwa bodi ya Ligi.
Na bodi ya Ligi imezipeleka wapi fedha
hizo? “Fedha za Yanga SC zipo, tumeziweka
katika akaunti maalum, za msimu uliopita
na msimu huu, wakizihitaji wakati wowote
waziandikie barua ya kuziomba,
tuwapatie,”amesema Mtendaji Mkuu wa
Bodi ya Ligi, Silas Mwakibinga.
Maana yake- kama Yanga SC wanazihitaji
fedha hizo wanaweza kuzipata ndani ya wiki
moja- iwapo wataandika barua na fedha
zitahamishiwa kwenye akaunti yao, au
kupewa hundi moja kwa moja.
Azam Media Limited waliingia Mkataba wa
haki za matangazo ya Televisheni ya Ligi
Kuu mwaka jana na TFF kwa pamoja na
bodi ya ligi hiyo, wakitoa Sh. Milioni 100
kwa kila klabu, wakati mwaka huu kuna
ongezeko la asilimia 10, na kufanya dau la
Milioni 110.
Tayari kwa msimu huu kila timu, kati ya 14
zilizopo kwenye ligi hiyo imekwishaptiwa
Sh. Milioni 55, wakati Sh. Milioni 55
nyingine zitatolewa sambamba na mzuguko
wa pili wa Ligi Kuu mapema mwakani.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment