Mtangazaji wa kipindi cha ‘Mboni Show’, Mboni Masimba
Jumatano hii kwenye viwanja vya Karimjee alifuturisha watoto yatima
kutoka kwenye vituo vitano vya mkoa wa Dar es Salaam.
Futari hiyo ilihudhuriwa na Makamu wa Rais, Samiah Hassan Suluhu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Mufti mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Salum, Mabalozi wa nchi mbalimbali, watu maarufu pamoja na wageni wengine waalikwa.
Akihutubia mara baada ya futari hiyo, Mboni alieleza kuwa, wamekuwa wakifanya hivyo mara kwa mara hii ni kutokana na kurudisha fadhila kwa jamii kwa kidogo kinachopatikana hivyo amewaomba wadau wengine kujitokeza kufanya jambo kama hilo kila inapohitajika kwa jamii.
Aidha Mama Samia alimpongeza Mboni kwa tukio hilo kuwa ni la kuigwa hivyo ni lazima jamii imuunge mkono kwa kujilea kwake.
Futari hiyo ilihudhuriwa na Makamu wa Rais, Samiah Hassan Suluhu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Mufti mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mussa Salum, Mabalozi wa nchi mbalimbali, watu maarufu pamoja na wageni wengine waalikwa.
Akihutubia mara baada ya futari hiyo, Mboni alieleza kuwa, wamekuwa wakifanya hivyo mara kwa mara hii ni kutokana na kurudisha fadhila kwa jamii kwa kidogo kinachopatikana hivyo amewaomba wadau wengine kujitokeza kufanya jambo kama hilo kila inapohitajika kwa jamii.
Aidha Mama Samia alimpongeza Mboni kwa tukio hilo kuwa ni la kuigwa hivyo ni lazima jamii imuunge mkono kwa kujilea kwake.
Aidha, Mama Samia Suluhu amesema serikali inaendelea kuvisimamia kwa ukaribu vituo vyote vya kulelea watoto yatima nchini na vituo ambavyo vitabainika kuwa vinanufaisha wamiliki na vinaendeshwa bila ubora vitafungiwa mara moja.
Makamu wa Rais amesema kuwa azma ya serikali ni kuona vituo vyote vya kulelea watoto yatima kote nchini vinatoa huduma bora na inayokidhi mahitaji ya watoto hao na sio vinginevyo.
Aidha, Mama Samia ameiomba jamii kuweka mipango mizuri ya kukabiliana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto yatima kwa kuwa nao wana haki ya kuishi vizuri kama watoto wengine.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment