Vanessa Mdee
Msanii wa muziki, Vanessa Mdee anayefanya vizuri katika soko la muziki
nchini Tanzania ameendelea kuwa na wiki ya kihistoria ambayo ilianza
kwa kuzindua albamu yake mpya iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa na
mashabiki wake na wadau wengine wa mziki nchini siku ya Jumatatu.
Ijumaa hii Vanessa amezindua programu ‘app’ yake mpya ya simu ya VEE
MONEY ambayo inapatikana bure kupitia ‘Google Play store’ na ‘Apple
store’. Programu hii ambayo imetengenezwa na kampuni ya masuala ya
teknolojia ya Marekani, Converge Media, ni sehemu ambayo mashabiki wa
Vanessa watakuwa wanapata maudhui ya kipekee ya Vanessa kama vile;
nyimbo, video, picha, na kuona kurasa zake za kijamii.‘Kwanza natoa shukrani za dhati kwa mashabiki wangu kwa kuipokea albamu yangu kwa mikono miwili, na sasa natumaini app hii itazidi kutuweka karibu,” alisema Vannesa.
Vanessa atakamilisha wiki yake ya kihistoria kesho kwa kuweka sahihi katika albumu zake tukio ambalo litafanyika eneo la Mlimani City Mall kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 12 jioni
0 MAONI YAKO:
Post a Comment