January 30, 2016


 
Hatimaye mwili wa mtu mmoja umepatikana ukiwa unaelea kandokando ya mto Kilombero takribani kilometa 5 kutoka eneo kilipozama kivuko cha mto kilombero januari 27 mwaka huu majira ya saa moja na nusu usiku.

Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard  Paul amesema kupatikana kwa mwili huo ni jitihada zinazoendelea kufanyika  kivukoni hapo kuhakikisha iwapo kuna miili mingine iliyozama inaopolewa  .

Kamanda amemtaja jina la marehemu ayeopolewa kuwa ni  Novatus Namali aliyekuwa mlinzi  wa kampuni  ya ulinzi ya RAFA  ya mjini Ifakara, ikielezwa kuwa serikali inatarajia kutumia helkopta ili kusaidia katika uokoaji  .

Mwili wa aliyekuwa  mlinzi wa kampuni ya ulinzi ya RAFA  Novatus Namali , umeleta matumaini  kwa wananchi wanaosubiri kupatikana kwa miili ya ndugu na jamaa zao  waliozama kwenye ajali ya kivuko januari 27 mwaka huu.

Pia Kamanda huyu ametoa onyo kwa vyombo vya habari juu ya  upotoshaji wa taarifa za tukio hilo.

 Katika hatua nyingine , Melikioli Mwangi , mzazi wa mtoto  aliyekuwa mtumishi wa benki ya  CRDB Dastun Rwegasira ambaye hajapatika mpaka sasa amesema anasikitishwa sana na tukio hilo kwani limemfanya kuwa katika wakati mgumu

 Pia mzazi huyu ametoa wito kwa mamlaka zinazohusika , juu ya  uendeshaji wa vivuko nchini kufanya uchunguzi wa kina kabla chombo hakijaanza safari ili kuweza kuepusha madhara na kusababisha vifo kama hivyo vilivyotokea.

Kivuka cha kilombero 2 kimezama januari 27 mwaka huu majira ya saa moja na nusu usiku kikiwa na abiria  ambao idadi yao haikufahamika , magari matatu, pikipiki na ,baskeli  pamoja na mizigo mingine  yakiwemo magunia ya mpunga.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE