Salaam Ndugu zangu wote mashabiki na wadau wa muziki wetu!!
Tamko langu kuhusiana na lugha zilizotolewa na Twent Percent kuhusiana na show yetu ya Zanzibar Music Award.
"Tulialikwa kwenye ZANZIBAR MUSIC AWARD, na kabla ya kazi makubaliano
yote ya kazi kwa mujibu wa mkataba yalifuatwa, makubaliano hayo
yalihusisha sisi kujigharamia gharama zote za nauli na Malazi
(accomodation).
Tulifika Zanzibar salama,
tulipokua Zanzibar twenty alitaka agharamiwe huduma zote ambazo ni nje
ya mkataba wetu, nikamuomba na kumsihi sana Ndugu yangu aheshimu
mkataba, asitafute matatizo kwani tayari mpaka wakati huu tuna kesi na
Halmashauri ya Manispaa ya Moro ambayo kimsingi sikuhusika (nilishatolea
ufafanuzi siku za nyuma).
Lakini yeye alipingana na mimi,
akanibishia na kunisukuma Mbele ya wageni na wenyeji wetu, wakiwemo
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seiph Ali Idi, Waziri Seiph
Khatibu.
Walikuwepo waadishi wa habari wa siku Nyingi Akiwemo
Abubakari Liongo (idhaa ya kiswahili radio Ujerumani), Mkurugenzi wa
ZENJI FM ndugu Tua Saidi Tua.
Mimi Selemani Abdallah Juma Msindi
sihusiki kwa namna yoyote, na tabia zisizo za kuridhisha zinazoonyeshwa
na Ndugu yangu Twenty Percent, ambae nimekua nae nyumbani kwangu hata
kabla ya Tuzo zake Tano (Kili Music Award) ambazo kazi hizo zote hizo
kaandikia nyumbani kwangu siwezi kuwa na tatizo nae ni ndugu yangu
kiimani na kikazi, hata kazi yangu niliyofanya nae kabla siku za nyuma
"MBELE YAKO NYUMA YANGU" .. Kuna mstari Nilisema " ..Kuandika Rhyme
kwenda Gym kimtindo kuonyesha Ugum, bado unatakiwa uwe na nidhamu ya
kweli, sio ya kumzuga Mwalimu, utajihukumu".
Nimekua nikisisitiza
nidhamu kwa Ndugu zangu woote toka enzi za Ghetto BoyZ, Watupori na
Mabwasha'Kingdom, ambao wengine hawafanyi sanaa, ila nipo nao kwenye
Familia yetu kubwa hapa Tanzania. Nimesikitishwa na kitendo hicho. Siku
zote nimekua mwenye kuhitaji suluhu kwa namna ya Amani.
Verry sorry
kwa wote ambao mumefadhaika kwa hilo. Tuendelee kuwa pamoja na msisite
kutoa ushauri wenu, maoni ili Game letu lisonge. MUNGU ATUBARIKI.
Asanteni sana.
Selemani Juma Abdallah Mutabhazi Msindi.
a.k.a Afande Sele (King of Rhymes)
Tamko langu kuhusiana na lugha zilizotolewa na Twent Percent kuhusiana na show yetu ya Zanzibar Music Award.
"Tulialikwa kwenye ZANZIBAR MUSIC AWARD, na kabla ya kazi makubaliano yote ya kazi kwa mujibu wa mkataba yalifuatwa, makubaliano hayo yalihusisha sisi kujigharamia gharama zote za nauli na Malazi (accomodation).
Tulifika Zanzibar salama, tulipokua Zanzibar twenty alitaka agharamiwe huduma zote ambazo ni nje ya mkataba wetu, nikamuomba na kumsihi sana Ndugu yangu aheshimu mkataba, asitafute matatizo kwani tayari mpaka wakati huu tuna kesi na Halmashauri ya Manispaa ya Moro ambayo kimsingi sikuhusika (nilishatolea ufafanuzi siku za nyuma).
Lakini yeye alipingana na mimi, akanibishia na kunisukuma Mbele ya wageni na wenyeji wetu, wakiwemo Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seiph Ali Idi, Waziri Seiph Khatibu.
Walikuwepo waadishi wa habari wa siku Nyingi Akiwemo Abubakari Liongo (idhaa ya kiswahili radio Ujerumani), Mkurugenzi wa ZENJI FM ndugu Tua Saidi Tua.
Mimi Selemani Abdallah Juma Msindi sihusiki kwa namna yoyote, na tabia zisizo za kuridhisha zinazoonyeshwa na Ndugu yangu Twenty Percent, ambae nimekua nae nyumbani kwangu hata kabla ya Tuzo zake Tano (Kili Music Award) ambazo kazi hizo zote hizo kaandikia nyumbani kwangu siwezi kuwa na tatizo nae ni ndugu yangu kiimani na kikazi, hata kazi yangu niliyofanya nae kabla siku za nyuma "MBELE YAKO NYUMA YANGU" .. Kuna mstari Nilisema " ..Kuandika Rhyme kwenda Gym kimtindo kuonyesha Ugum, bado unatakiwa uwe na nidhamu ya kweli, sio ya kumzuga Mwalimu, utajihukumu".
Nimekua nikisisitiza nidhamu kwa Ndugu zangu woote toka enzi za Ghetto BoyZ, Watupori na Mabwasha'Kingdom, ambao wengine hawafanyi sanaa, ila nipo nao kwenye Familia yetu kubwa hapa Tanzania. Nimesikitishwa na kitendo hicho. Siku zote nimekua mwenye kuhitaji suluhu kwa namna ya Amani.
Verry sorry kwa wote ambao mumefadhaika kwa hilo. Tuendelee kuwa pamoja na msisite kutoa ushauri wenu, maoni ili Game letu lisonge. MUNGU ATUBARIKI.
Asanteni sana.
Selemani Juma Abdallah Mutabhazi Msindi.
a.k.a Afande Sele (King of Rhymes)
0 MAONI YAKO:
Post a Comment