Kwenye Refresh ya Wasafi Tv, Dee
amekazia kuwa siku zote wanawake wanajua Marioo anataka nini, hivyo
mpenzi wake Janjaro amejua Jamaa anapenda viatu,nguo mpya na kusafiri na
ndicho anacho kifanya hadi Dogo Janja kasahau kitu kinaitwa muziki.😁
August 07, 2022
- 1:29 AM
- Machaku
- No comments
Sekretarieti ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imewafungulia mashtaka ya kimaadili Rais wa Yanga, Mhandisi Hersi Said na aliyekuwa Ofisa wa Klabu hiyo Haji Manara “Kamati ya Maadili ilimfungia miaka miwili Manara kujihusisha na shughuli yoyote ya mpira wa miguu lakini ameshindwa kutekeleza adhabu hiyo”
Kamati
imesema Hersi amefunguliwa mashtaka kwa kwenda kinyume na ibara ya
16(1) (a) ya Katiba ya TFF pamoja na ibara ya 1(6) ya Katiba ya Yanga.
Taarifa
ya TFF:
Baada ya Manara kuadhibiwa na Kamati ya
Maadili ya TFF, Sekretarieti ilimwandikia barua Mhandisi Said
kuhakikisha Klabu yake inaheshimu uamuzi huo, Mwenyekiti wa Kamati ya
Maadili tayari amepelekewa mashtaka hayo, walalamikiwa watapewa mashtaka
na mwito mara baada ya Kamati kupanga tarehe ya kusikiliza mashtaka
hayo”.
- 1:18 AM
- Machaku
- No comments
KUMBUSHO LA HARAKA!
Mwaka jana mlipoteza mechi siku ya mwananchi, lakini mliendelea kushinda michezo yote mbele na kutwaa vikombe vyote nchini. Ilinisikitisha sana kiasi kwamba wakati mwingine nikienda kwenye kidimbwi na kuomba kikombe kwa ajili ya kinywaji changu,
- 1:03 AM
- Machaku
- No comments
Karibu mpenzi wa Machaku Media katika kurasa za Magaazetini leo hii. Leo ni siku ya jumapili 07 August 2022. Tumekukusanyia baadhio ya kurasa za Magazetini zilizotufikia katika Meza yetu hapa STUDIO. Kwa taarifa za kina katika kurasa za Magzetini, fika katika Meza iliyo karibu nawe ujipatie nakala yako sasa.
- 12:31 AM
- Machaku
- No comments
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akimkabidhi cheti
cha pongezi Mkurugenzi Msaidizi wa Kuzuia Ujangili, Wizara ya Maliasili
na Utalii, Bw.Robert Mande (kulia) kwa kushiriki katika utoaji mafunzo
ya kukabiliana na ujangili na usafirishaji haramu wa mazao ya
wanyamapori na mimea ndani na nje ya Bara la Afrika uliofanyika leo
jijini Dar es Salaam.
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akifunga mafunzo
ya siku tano ya kukabiliana na ujangili na usafirishaji haramu wa mazao
ya wanyamapori na mimea ndani na nje ya Bara la Afrika uliofanyika leo
jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Kuzuia Ujangili, Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw.Robert
Mande (kulia) akizungumza na washiriki wa mafunzo ya kukabiliana na
ujangili na usafirishaji haramu wa mazao ya wanyamapori na mimea ndani
na nje ya Bara la Afrika uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akimkabidhi cheti
cha pongezi Afisa Uwajibikaji na Mkurugenzi wa Haki wa Taasisi ya Grace
Farm Foundation Rob Khattabi (kulia)kwa kushiriki katika utoaji mafunzo
ya kukabiliana na ujangili na usafirishaji haramu wa mazao ya
wanyamapori na mimea ndani na nje ya Bara la Afrika uliofanyika leo
jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Kuzuia
Ujangili, Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw.Robert Mande (kushoto)
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) (katikati
waliokaa) katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mafunzo ya
kukabiliana na ujangili na usafirishaji haramu wa mazao ya wanyamapori
na mimea ndani na nje ya Bara la Afrika uliofanyika leo jijini Dar es
Salaam.
Baadhi
ya washiriki wa mafunzo ya siku tano ya kukabiliana na ujangili na
usafirishaji haramu wa mazao ya wanyamapori na mimea ndani na nje ya
Bara la Afrika wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.
Mary Masanja (Mb) (hayupo pichani)akifunga mafunzo hayo leo jijini Dar
es Salaam.
June 21, 2021
January 16, 2020
- 12:46 PM
- Machaku
- No comments
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mhe. Abdulaziz Abood (CCM) akiangalia namna mashine ya X-ray ya kisasa inavyofanya kazi katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro.
Kufuatia kilio cha muda mrefu cha wakazi wa mkoa wa Morogoro juu ya kukosekana kwa mashine ya X-ray ya kisasa katika hospitali ya rufaa ya mkoa huo hali iliyokuwa ikiwalazimu kupewa rufaa kwenda hospitali ya taifa Muhimbili kwa ajili ya Matibabu hatimaye Serikali imesikia kilio chao na kupeleka mashine hiyo ya kisasa kama ilivyoahidi.
Akiendelea na ziara ya kutembelea hospitali ya Rufaa ya Morogoro na vituo vya afya katika manispaa ya Morogoro leo Alhamis Januari 16,2020, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mhe. Abdulaziz Abood (CCM) amejionea mashine hiyo ikifanya kazi.
Mhe. Abood ameishukuru serikali kwa kutekeleza ahadi yake hiyo na kuwajali wananchi wa mkoa wa Morogoro kwa kuleta mashine ya kisasa kwa ajili ya huduma za X-ray kwani kilikuwa ni kilio cha muda mrefu ambacho amekuwa akiiomba Serikali kuwasaidia kifaa hicho.
Mhe. Abood amesema mara kadhaa amekuwa akiomba kupatiwa mashine hiyo hata akiwa bungeni na amemshukuru Rais Magufuli kwa kusikiliza ombi hilo maalum na kuwapatia mashine hiyo ya X-ray ya kisasa.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro,Dkt.Ritha Lyamuya amesema mashine hiyo imekuwa msaada mkubwa kwao kutokana na kuwa na uwezo mkubwa wa kazi hali ambayo amesema imesaidia hata kupunguza malalamiko ya wagonjwa ambao walikuwa wakikosa huduma ya X-ray kutokana na mashine iliyokuwepo awali kutokuwa na uwezo wa kufanya kazi.
Dkt. Lyamuya amesema mashine hiyo ina uwezo mkubwa wa kufanya kazi na hivyo kusaidia hata kupunguza idadi ya wagonjwa ambao walikuwa wakipewa rufaa kwenda hospitali ya taifa muhimbili kwani mashine hiyo ina uwezo wa kutuma taarifa za mgonjwa kwa njia ya mtandao na kurejesha majibu ndani ya muda mfupi.
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mhe. Abdulaziz Abood (katikati) akipokea maelezo namna mashine ya X-ray ya kisasa inavyofanya kazi katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro.
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mhe. Abdulaziz Abood (katikati) akipokea maelezo namna mashine ya X-ray ya kisasa inavyofanya kazi katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro.
December 01, 2019
- 3:11 AM
- Machaku
- No comments
Baada ya Bondia Twaha Kiduku wa Morogoro kutangaza hadharani akitaka mpambano na Bondia kutoka Dar Es Salaam Dulla Mbabe, sasa ni rasmi. Promota Ally Mwanzoa wa Tanga, ametaka mabondia hao kukutana naye na kuandaa pambano kati yao. Promota Mwanzoa amewapa Uhuru mabondia hao kuipanga tarehe na mwezi watakaotaka kupigana ila waende mezani wakaini mikataba ya pambano hilo.
Bondia Twaha Kiduku alipokewa kishujaa Mkoani Morogor, kufuatia mapokezi aliyoandaliwa wakati akireje mkaoni hapa baada ya kumtwangwa vilivyo bondia kutoka Afrika Kusini France Thabang Ramabolu katika pambano la utangulizi la mchuano uliowakutanisha Hassan Mwakinyo kutoka Tanzania na Arnel Tinampay kutokea Philipino mpambano ambao ulimalizka kwa Hassan Mwakinyo kuibuka mbabe kwa Point.
Twaha aliwasili Morogoro mida ya saa nane mchana na kupokewa na mamia ya wakazi wa Mji wa Morogoro na kusababisha baadhi ya shughuli kusimama kwa muda. Akizungumza nasi katika mapokezi hayo, mratibu wa mapokezi hayo Jackson Jackson Charles Busanda amesema amefurahishwa na muitikio mkubwa wa wakazi wa Morogoro licha ya kuandaa tukio kwa muda mfupi. Naye kwa upande wake Bondia Twaha amewashukuru wakazi wa Morogoro kwa mapokezi yale na kusema hana cha kuwalipa zaidi ya kuwawakirisha vema katika mashindano mengine. #hongera sana Twaha Kiduku
November 24, 2019
- 6:25 AM
- Machaku
- No comments
- 3:59 AM
- Machaku
- No comments
Official Video ya mwanamuziki mkali wa Free Style kutokea mkoani Morogoro Rajram
(RAJRHYMES ) imekamilika na nipo hewani nkwa ajili yako shabiki na mdau wake .
November 14, 2019
Subscribe to:
Posts (Atom)