
Waziri Nchimbi kwanza alitoa ufafanuzi wa wahamiaji hao haramu ili kuondoa mkanganyiko unaoenezwa kwamba Tanzania imeamua kufukuza raia wa mataifa jirani.
Alisema wanaotakiwa kuondoka ni wale wanaoishi nchini kinyume na sheria ya uhamiaji inayowataka kuomba vibali maalum vya ukaazi na ufanyaji kazi hapa nchini
Kuna madai pia kwamba wahamiaji haramu walioamua kuondoka kwa hiari yao baada ya agizo la mkuu wa nchi Rais Jakaya Kikwete hivi karibuni, hawatendewi haki wengi wanaporwa mali zao na kufanyiwa uhuni.
Waziri wa mambo ya ndani amesema kufanya hivyo ni kosa kisheria na ndiyo sababu wametoa agizo la wahamiaji wanaotaka kuondoka na mali zao watoe taarifa kwa vyombo vya usalama ili polisi wawasindikize mpaka mpakani.
Wahamiaji haramu 10,672 wameshaondoka nchini Tanzania kuanzia kutangazwa kwa operesheni hiyo na Rais mwishoni mwa mwezi julai mwaka huu.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment