NMB ikiwa ni benki ya chaguo la watanzania wengi,sasa basi taarifa njema ni kwamba (14 Sept) imezindua rasmi kampeni kabambe ‘Weka na Ushinde’ ambayo itakushawishi wewe mteja kuweka fedha benki ili uweze kujipatia ushindi ambao si wa Bajaji,Bodaboda,Baiskeli au fulana za NMB tu bali pia faida kubwa ya riba na usalama wa pesa zao.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika uzinduzi huo Meneja wa Amana za wateja katika benki hiyo Bw.Boma Raballa amesema kwamba kampeni hiyo itafanyika katika kipindi cha miezi mitatu kuanzi sasa mpaka Desemba 29,2014
Zawadi hizo zinathamani ya zaidi ya TZS 500 Milioni ambazo ni (Bajaji-52,Bodaboda-52,Baiskeli-400 na fulana-500).
Watanzania wote mnaweza kushiriki na nirahisi kwa mteja aliye na akaunti anahitaji kuweka TZS 50,000 kama kiwango cha chini na yule asiye na akaunti anahitaji kufungua akaunti NMB ili aweze kuweka aghalau TZS 50,0.00 kama kiwango cha chini ili aweze kuingizwa kwenye droo ya Bahati Nasibu.
Naye Meneja wa Kanda jijini Dar es Salaam Salie Mlay amesema kwamba zawadi hizo zitatolewa kwenye matawi yote 150 yaliyopo nchini hii ni fursa kwa wananchi kuweza kufaidika na kampeni hiyo.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment