November 01, 2014

Hapa Nay akiwa na Mlezi wa kituo hicho
 Katika hali isiyo ya kawaida kwa wasanii wa hapa Tanzania, ni wachache sana wenye moyo kama huo wa Nay wamitego.

 Msanii Nay wa mitego ametoa asilimia kumi ya pato lake alilolipata katika Show za Serengeti Fiesta 2014 na kupeleka kwa watoto yatima. 
 Akizungumza na Ublaozini.blogspot.com Nay amesema ameamua kufanya hivyo kwa sababu anayajua mazingira wanayoishi wale watoto na jukumu la kuwasaidia si la tahasisi fulani au Serikali bali ni jmukumu letu sisis sote
Baadhi ya watoto wanaolelewa kituoni hapao.
 Tukio hilo lilifanyika siku ya Jumatato Trh 29 0ct 2014 katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Mwandaliwa Orphans cha Jijini Dar Es Salaam
Nay akiw na watoto yatima
  "Unajua nimeamua kufanya hivi kwa sasabu, wale watoto hawakutamani yale maisha wanayoishi katika mazingira yale, kuondokewa na baba au mama ni jambo zito sana katika ulimwengu hasa kwa mtoto asiyejua lolote. Walitamani kuishi na wazazi wao miaka yote lakini haikuwa hivyo. Wanaumia sana na ndiyo maana nimeonelea kile kidogo nilichopata nigawane nao, leo yule kesho atakuwa mwanagu halina mmoja lile. Kwa hiyo nimependa kufanya vile ili kuona kwamba watambue tupo nao pamoja, wasiumie sana. Lile swala ni la jamaii nzima siyo serikali au taasisi ndiyo inayohitajika kuwahudumia, bali kila mwenye kujua uchungu wa mzazi na ata yeyote ajue ni wajibu wake pia"



 Hapa akikabidhi baadhi ya vifaa

Baadhi ya watoto wakiwa na nyuso za Furaha na kaka yao

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE