Mara nyingi tumesikia kwamba mwanamke akiwa mjamzito huwa kuna kitu
anapendelea kula kuliko vitu vingine lakini hii inaweza kukushangaza
zaidi kwani.
Mwanamke mmoja Jade Sylvester mama wa watoto watano amethibitisha kuwa anashindwa kujizuia kula toilet paper kila siku.
Jade amesema alianza kutamani kula wakati akiwa na ujamzito wa miezi miwili wa mtoto wake wa kiume Jaxon, lakini hadi sasa bado anaendelea kula na amekuwa akila kila siku lakini hajui kinachopelekea apendelee kula.
Pamoja na kujifungua mtoto wake wa kiume miezi 15 iliyopita Jade
hawezi kukaa mbali bila kula karatasi hizo na kuna wakati ambao hujikuta
akila bunda zima kwa wakati mmoja japo havutiwi na ladha yake, ila
anavutiwa zaidi na ulaini wa karatasi hizo.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment