January 27, 2015

 
 Mwanamuziki Ray C ambae alitamba miaka ya nyuma na ngoma kali kibao ikiwemo Na wewe milele,Sogea sogea na nyingine nyingi amefunguka na kusema kuwa kwa sasa hakuna mtu atakae weza kutembelea nyota yake katika muziki kwani sasa maisha yake
ameyakabidhi kwa Mwenyezi Mungu ambaye ndiye mlinzi wake na mwongozaji wake katika maisha,Ray C amefunguka hayo kupitia ukurasa wake wa Instragram.
"Tatizo Nyota.........Kwa sasa ameishikilia Mola wangu pekee hakuna atakaeitembelea tena! !!!!!!!!MSHUMMSHUM"
Mwanamuziki Ray C ambae alikuwa kimya kwa muda mrefu katika tasnia ya muziki alipatwa na matatizo ya utumiaji wa madawa ya kulevya ambayo kwa namna moja au nyingine ndiyo yalifanya awezekupotea katika tasnia hata kuchangia pia kwa baadhi ya mambo yake ya maendeleo kushindwa songa lakini baadae mwanamuziki huyo aliweza kutoka katika mtego huo kwa kuacha kabisa kutumia madawa ya kulevya na kuwa mwanaharakati tena mstari wa mbele kuwaokoa wasaniii wengine ambao nao walitumbukia katika matumizi ya dawa za kulevya.
Ray C ameweka wazi kuwa katika kipindi ambacho yeye alikuwa na matatizo kuna kundi la watu au baadhi ya watu walikuwa wanafurahia na hawakupenda kwa mwanamuziki huyo kumwona anachomoka katika matatizo ambayo yalikuwa yanamsonga yakiwemo ya matumizi ya dawa za kulevya na pia hawakupenda kuona mwanamuziki huyo anarudi katika muziki kama ilivyokuwa awali,bali walitamani hata angekufa kwa matumizi ya dawa za kulevya,haya yote amefunguka leo.
"Nakuona wewe hapo,najua unanichukia na unatamani ningefia mbali na uteja!Unatamani nisingepona! Unatamani nisingerudi kwenye muziki wewe apo! Pole mwaya Mungu hajapenda niondoke so talk to my....... coz my face doesn't wanna see u"
Katika siku za hivi karibuni Ray C amekuwa katika mkakati kabambe wa kupunguza mwili wake ili aweze kurejea katika hali yake ya kawaida ambayo zamani ilikuwa ikiwashika watu na kufanya watu kumpatia jina la kiuno bila mfupa kutokana na uwezo wake stejini na kuweza kucheza na mwili wake.
Ray C ni miongoni mwa wasanii wa zamani katika game ya bongo fleva ambao bado wana nia na hamu ya kuona wanarudi katika muziki na kushindana na soko la muziki wa sasa.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE