Rubani wa ndege ya kampuni ya
Germanywings ilioanguka katika milima ya Alps nchini Ufaransa siku ya
jumanne alitaka kuiharibu ndege hiyo kulingana na maafisa wa
Ufaransa.Kiongozi wa mashtaka katika mji wa Mersaille ,Brice Robin,
akizungumza kulingana na habari aliyopata katika kijisanduku cha kunasa
sauti katika ndege amesema kuwa rubani huyo alikuwa ndani ya chumba cha
kuendesha ndege pekee.
Rubani huyo kimakusudi aliishusha ndege hiyo kwa kasi huku rubani mwenza akiwa nje ya chumba hicho cha kuendesha ndege.Bwana Robin amesema kuwa kulikuwa na kimya kikubwa ndani ya chumba hicho wakati rubani mwenza alipojaribu kuingia kwa nguvu.
Hatahivyo abiria walisikika wakipiga nduru kabla ya kuanguka kwa ndege hiyo,aliongezea.
Rubani huyo kwa jina Andreas Lubtiz,mwenye umri wa miaka 28, alikuwa
hai hadi wakati ndege hiyo ilipoanguka ,kiongozi wa mashtaka alisema.
Ndege
hiyo aina ya Airbus 320 iliokuwa ikitoka Barcelona kuelekea Duesseldorf
Ujerumani iligonga mlima na kuwauwa abiria wote 144 pamoja na
wafanyikazi sita wa ndege baada ya kushuka kwa dakika nane.
"Tunasikia
rubani akimuuliza rubani mwenza kuchukua udhibiti wa usukani wa ndege
hiyo na vilevile tunasikia sauti ya kiti kikisonga nyuma na mlio wa
mlango ukifungwa,bwana Robin aliwaeleza wanahabari.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment