April 17, 2015

Waislamu TZ watakiwa kujiepusha na uvunjaji amani
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini, Ernest Mangu na viongozi wa dini ya Kiislamu nchini, wameungana kwa pamoja na kukemea vitendo vya uhalifu. Viongozi hao wamezitaka familia kutoa malezi bora kwa watoto wao ili kuondokana na wimbi la watu wanaojiingiza katika vitendo hivyo. Mkuu wa Jeshi la Polisi Inspekta Jenerali Mangu amesema viongozi wa dini wana dhamana kubwa katika kuhakikisha vitendo vya uhalifu vinadhibitiwa nchini kwa kuwaelimisha waumini wao na jamii kwa ujumla juu ya madhara ya uhalifu.
Mwakilishi wa Mufti Mkuu wa Tanzania katika kikao hicho ambaye ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Ulamaa katika Baraza Kuu la Waislamu Nchini (BAKWATA), Sheikh Abubakar Zuberi alisema kuna haja ya kuziba nyufa za uvunjifu wa amani, ambazo zimeanza kujitokeza nchini.
Naye Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Khamis Mataka alisema uhalifu unaweza kujitokeza sehemu yoyote na hata ndani ya msikiti, hivyo ni jukumu la viongozi wa misikiti kuwafichua wahalifu walio ndani ya misikiti.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE