Ripoti kutoka Nigeria zinasema kuwa
wanafunzi watatu wa chuo kimoja cha mafunzo ya biashara, wameuwawa na
wapiganaji wa Boko Haram, pale chuo chao kilipovamiwa kazkazini
mashariki mwa Nchi hiyo.
Wengine kadhaa walipata majeraha mabaya
ya risasi, pale watu wanaoaminika kuwa wa kundi la wanamgambo wa Boko
Haram, walipovamia chuo chao na kuanza kumina risasi kiholela.Mmoja wa washambuliaji alifariki alipojilipua nje ya lango la chuo hicho, nje kidogo ya mji wa Potiskum katika jimbo la Yobe.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment