July 01, 2015

 Watu wanne wamefariki dunia na 21 kujeruhiwa baada ya basi aina ya Isuzu  kugonga treni ya abiria iendayo bara katika  kilomita 276/0 kati ya Stesheni  za Kimamba na Kilosa mkoani Morogoro saa 11:25 asubuhi leo Julai 01, 2015. Wahanga walipakiwa katika  treni hiyo na kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa.
Basi lilohusika ni lenye namba za usajili T837CTM Isuzu Coaster linalomilikiwa na Feisal  A. Khuwel wa Kilosa.Taarifa kutoka eneo la tukio  limefafanua kuwa waliofariki ni wanaume wawili, mwanamke mmoja na mtoto wa miaka minne. Katika majeruhi 21 wako wanaume 14 na Wanawake 7 ambao wanaendelea na matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa! Treni ya abiria imeondoka katika Stesheni ya Kilosa saa 3 asubuhi  kuendelea na safari yake kwenda Bara. Uongozi wa TRL  unawapa pole Ndugu wa Marehemu  kwa msiba mkubwa uliowakuta bila ya kutarajiwa na pia inawaombea Marehemu  kwa Mola  awape mapumziko ya Amani peponi Amina! Hali kadhalika inawaombea majeruhi wapate afueni ya haraka ili warejea katika shughuli zao za kawaida kwa familia zao na Taifa letu.

Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL Mhandisi Elias Mshana Dar es Salaam! Julai 01, 2015




0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE