Viongozi wa dini mkoani Mtwara wamewataka waandishi wa habari kutimiza wajibu wao kwa kuielisha jamii namna ya kuishi na kutenda haki ili kudhibiti vitendo vya kifisadi vinavyofanywa na baadhi ya watu.Ustadh Jafari Atiki, kutoka katika taasisi ya Darul Hadith Islamic
Akizungumza
jana , Mchungaji Zakaria Lyakungi, kutoka Kanisa la Kiinjili la
Kilutheli Tanzania, jimbo la Pwani, amesema ni wajibu wa waandishi
kuikemea jamii bila woga iwapo kutakuwa na vitendo viovu.
Kwa upande wake, Ustadh Jafari Atiki, kutoka katika taasisi ya Darul
Hadith Islamic, amesema waandishi wa habari ni kama viongozi wa dini kwa
namna wanavyoaminiwa na jamii, hivyo hawatakiwi kuegemea upande wowote
katika ufanyaji wa kazi zao.
Naye, makamu mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa
Mtwara (MTPC), Jimmy Mahundi, amewasisitiza waandishi kujihepusha kuwa
chanzo cha matatizo na baadala yake kuwa msaada kwa jamii inayokumbwa na
matatizo na kuhitaji msaada wao.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment