December 30, 2015


Rais wa Jamburi ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa Makatibu wakuu na Manaibu Katibu wakuu wa wizara mbalimbali.

Aidha, Rais Magufuli pia amemteua Eliakimu Maswi kuwa Kaimu Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na kutengua uteuzi wa Naibu Kamishina wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Lusekelo Mwaseba.

Miongoni mwa Makatibu walioteuliwa ni pamoja na nafasi ya Katibu Mkuu Kiongozi, ambaye amebaki Balozi Ombeni Sefue.

Baadhi ya Makatibu waku hao waliochaguliwa ni pamoja na Mhandisi Mussa Iyombewa ameteuliwa katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Ofisi ya Makamu wa Rais anakuwa Mbaraka A. Wakili.

Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano waliochaguliwa ni Mhandisi Joseph. Nyamuhanga (Katibu Mkuu – Ujenzi), Dokta Leonard M. Chamuliho (Katibu Mkuu - Uchukuzi) na Profesa Faustine R. Kamuzora (Katibu Mkuu - Mawasiliano).

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ni Dokta Yamungu Kayandabira, Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi ni Maimuna Tarishi.

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wanakuwa ni Dokta Mpoki Ulisubisya atakayesimamia Afya na Sihaba Nkinga - Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Wizara ya Nishati na Madini ni Profesa Justus W. Ntalikwa, Wizara ya Mambo ya Ndani ni Jaji Meja Jenerali Projest A. Rwegasira.

Wizara ya Fedha na Mipango anabaki kuwa Dokta Silvacius Likwelile , Wizara ya Mambo ya Nje, Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa ni Dokta Aziz Mlima. Huku Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa akiteuliwa Job D. Masima.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE