January 23, 2016

KATIBU Mkuu wa Yanga SC, Dk. Jonas Tiboroha (pichani kushoto) amejiuzulu leo na tayari amewasilisha barua kwa Mwenyekiti, Yussuf Mehboob Manji.
Tiboroha ameiambia BIN ZUBEIRY SPORTS – ONLINE kwamba amechukua uamuzi huo ilia pate muda zaidi wa kufanya shughuli zake za Uhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
“Mimi ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kitivo cha Elimu ya Viungo (PE), na kwa kuondoka Yanga SC maana yake napata wasaa mzuri wa kumtumikia mwajiri wangu, UDSM,”amesema.
Pamoja na Tiboroha kutozama ndani sana juu ya kujiuzulu kwake, lakini inaelezwa alikuwa hana maelewano na Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya klabu, Isaac Chanji ambaye kwa sasa ndiye mtu anayesikilizwa na kuaminiwa zaidi na Manji.
Juhudi za kumpata Chanji kuzungumzia kujiuzulu kwa Tiboroha hazikufanikiwa hadi tunapandisha habari hii, ingawa zinaendelea ili kupata maoni yake.Isaac Chanji (kushoto) akiwa na Mwenyekiti Yussuf Manji (kulia) na Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga (katikati)
Kwa upande wake, Tiboroha alipoulizwa kuhusu mahusiano yake na Chanji alisema; “Nilichoandika katika barua yangu ya kujiuzulu ndiyo sababu za msingi, kikubwa ninawapisha watu ambao wanaweza kuiongoza vizuri Yanga SC kuliko mimi,”amesema.
Tiboroha aliingia Yanga SC Desemba mwaka 2014 akichukua nafasi ya Benno Njovu aliyeondolewa kwa tuhuma mbalimbali. Aliingia Yanga SC akitokea Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kama Ofisa Maendelezo ya Ufundi.


Source:Binzubeiry

Related Posts:

  • Familia zaidi ya 30 Morogoro zakosa makazi Kaya 30 za kata ya Kilakala manispaa ya Morogoro hazina makazi baada ya nyumba zao kuzingirwa maji kufuatia mvua zilizo nyesha mda mfupi na kusababisha maji kuacha muelekeo baada ya kuziba mifereji ya kuyapitisha kisha kuing… Read More
  • Butiku "wazanzibar msikubali kurudia uchaguzi" Taasisi ya mwalimu Nyerere imeitaka tume ya uchaguzi ya Zanzibar ZEC kufanya kazi kwa kuzingatia katiba ya nchi na sheria na sio kutanguliza mbele maslahi binafsi ya kisiasa hatua ambayo inaweza kusababisha machafuko na umwa… Read More
  • Maafisa wa kituo cha kukusanya taarifa cha TACCEO wakamatwa Wakili Imelda – Lulu Urio Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC. Chanzo:MOE BLOG Mtandao wa Asasi za Kiraia za Kuangalia chaguzi nchini jana ulipata pigo katika mwendelezo wake wa kukusanya taarifa juu ya mchakato wa… Read More
  • Obama aing'oa Burundi Mshirikishe mwenzako Image copyrightAFPImage captionMarekani imeiondoa Burundi kutoka kwenye mikataba yake ya kibiashara AGOA iliyowezesha mataifa ya Afrika kuingiza bidhaa zao katika soko la Marekani bila kulipa kodi. Mare… Read More
  • Shindano kubwa la kusaka vipaji vya kuchezea mpira Tanzania Freestyle football championship (TFFC2016) ambalo  ni shindano la kutafuta/kusaka vipaji vya kuchezea mpira yaani freestyle soccer/Freestyle Football wengi hupenda kuita hivyo ambalo… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE