Leo mashabiki wa Arsenal wamefurahishwa na usajili wa mchezaji mpya na kuwaacha watani wao wa jadi wakisubiri taarifa za usajili kwenye club yao.
Taarifa iliyopo sasa hivi ni kwamba Manchester United wanakaribia kumsajili mchezaji kinda wa miaka 16 Luca Ercalani kutoka club ya Forli inayocheza Serie D.
Mchezaji huyu alionwa na scout David Williams na kupelekwa Manchester United kwa ajili ya trial na inasemekana ameshafuzu na hivi sasa zinafanyika hatua ya mwisho kukamilisha usajili wake.
Mtu ambae aliyem-scout mchezaji huyu aliwahi kuwaleta wachezaji kama Federico Machedo na Giuseppe Rossi. Wachezaji wote hawa waliweza kuonyesha kuwa ni tumaini kwa Manchester united wakiwa vijana lakini baadae walishindwa ku-shine.
Haitegemewi kufanyika tangazo rasmi la usajili wa mchezaji huyu lakini kwenye page zake za instagram anaonekana kufurahia kwa jinsi mambo yanavyoenda. Vyanzo vya karibu na habari hii vinasema kila kitu kitakamilika ndani ya muda mfupi ujao.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment