January 08, 2016

Mwongozo 
Mamlaka ya mawasiliano nchini Kenya imechapisha mwongozo mpya wa vipindi vya radio na televisheni.
Mwongozo huo unanuia kudhibiti nyakati za kupeperusha matangazo na vipindi vinavyolenga watu wazima na pia kuepusha matumizi ya lugha chafu na gumzo za ngono.
Mwongozo huo utakapotekelezwa pia utapiga marufuku kupeperushwa kwa vipindi vya kidini vyenye ujumbe wa kuomba pesa kwa waumini ili wapate baraka.
Mwaka uliopita, mhubiri mmoja aligonga vichwa vya habari baada ya makala ya ufichuzi kuonyesha akifanya miujiza bandia na kuwaomba watu wamtumie takriban $3 (£2) kupitia simu akisema ni baraka ndipo wapate baraka.
Hii ni mara ya kwanza hatua kama hiyo kuchukuliwa.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE