February 27, 2016


 

 Hivi karibuni kiungo wa kimataifa wa Kenya anayekipiga katika klabu ya Southampton Victor Wanyama alimtaja mwanamuziki wa kizazi Alikiba kwamba ndio muimbaji anyemkubali zaidi kutoka nchini Tanzania.

Kenya imeendelea kuwa moja ya eneo lenye soko kubwa kwa wasanii wa Bongo Fleva – na hii imeendelea kudhihirika baada ya mshambuliaji wa Liverpool, raia wa Belgium mwenye asili ya Kenya Divock Origi ameungana na Wanyama kwa kusema hakuna msanii wa muziki ndani ya mipaka ya Afrika Mashariki anayemkubali kama muimbaji wa wimbo ‘Lupela’ Alikiba.  


 
 Unajua mama yangu huwa ana CDs za muziki kutoka Kenya sana, napenda ngoma za Alikiba sana kuliko Diamond ama hao wengine,” alisema Origi, akiongea nyumbani kwake huko  Merseyside, United Kingdom na mwandishi wa Pulse Kenya.

  
 Alikiba pamoja na kuimba lakini mpenzi mkubwa wa soka akiwa anaishabikia Yanga pamoja na klabu anayochezea Origi – Liverpool.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE