March 09, 2016

seif-2 

Rais John Magufuli amemtembelea na kumjulia hali Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad, katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam, ambako anapata mapumziko baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali ya Hindu Mandal alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Pamoja na kumpa mkono wa pole, Rais Magufuli amemuombea Maalim Seif Shariff Hamad kupona haraka ili aweze kuendelea na shughuli zake kama kawaida.
Kwa upande wake Maalim Seif Shariff Hamad amemshukuru Rais Magufuli kwa ukarimu na upendo aliouonesha kwa kumtembelea hotelini hapo, na amewahakikishia watanzania kuwa hali yake sasa inakwenda vizuri na inazidi kuimarika
Maalim Seif alilazwa kwa siku kadhaa hospitali ya Hindu Mandal baada ya kuzidiwa wakati akitokea Zanzibar kuja Dar es salaam siku chache tokea kuwasili nchini akitokea nchini INDIA kwa matibabu.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE