
Basi hilo lenye usajili namba T 720 ADE lililigonga na lori hilo lenye usajili namba T742 CRS ambapo kwa mujibu wa Mashuhuda wa ajari hiyo ,wanadai ajali hiyo ilitokea majira ya saa tisa alfajiri wakati basi la Saibaba lilipokuwa likifanyiwa majaribio na fundi aliyejulikana kwa jina la Athuman sadiki naghafla lilizimika taa zote za mbele na kupoteza mwelekeo na ndipo lilipo ligonga lori hilo lillilokuwa limebeba shehena ya karoti.
Hata hivyo inadaiwa kuwa marehemu na majeruhi wote walikuwa abiria wa lori.
Channel ten inafanya jitihada za kufika katika hospital ya mkoa wa Arusha mount meru ambapo uongozi wa haspitali hiyo unashindwa kutoa ushirikiano wa aina yoyote licha ya majeruhi na miili ya marehemu kuripotiwa kufikishwa katika hospital hiyo huku kamanda wa jeshi lapolisi mkoa wa arusha Liberatus Sabasi akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na tayari dereva wa basi anashikiliwa na jeshi hilo.
Kwa mujibu wa kamanda Sabasi majina ya marehemu hao ni Nouvel Joseph ambaye ndiye alikuwa dereva wa lori hilo wengine ni ,james kaaya na paschal peter wote wakiwa abiria katika lori hilo.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment