May 05, 2016

Rufani ya aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ‘TRA’, Harry Kitilya, Sioi Solomoni na aliyekuwa afisa mwandamizi benki ya Stanibic tawi la Tanzania ambaye pia ni mshindi wa taji la Miss Tanzania 1996, Shose Sinare imesikilizwa leo Mahakama kuu.

Upande wa utetezi umedai kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo kwa kuwa mahakama ya hakimu mkazi kisutu haikumaliza kusikiliza kesi hiyo lakini upande wa serikali umesema haki wanayo kwa sababu shitaka la nane limeshamalizika.

Mahakama Kuu imeeleza kuwa kesho ndio itatoa uamuzi wa Rufani hiyo kama isikilizwe mahakamani hapo au la.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE