Awali iliripotiwa kuwa Shule Nane Kaskazini mwa Afrika Kusini zilichomwa na waandamanaji.
Maandamano nchini Afrika Kusini yana
historia ya kubadilika na kuwa ghasia, ikianzia miaka ya nyuma ya
utawala wa wakoloni ambapo wakaazi waliokasirika walikuwa wakiharibu
mali ya serikali kuonyesha kutopendelea jambo fulani.
Ni zaidi ya miaka 20 sasa tangu taifa hilo lijipatie uhuru wake na inaonyesha kuwa hatua hiyo haijasahaulika.
Watu hukasirishwa kwa kile wanasema ni
hali ya kujikokota kwa serikali kuwapatia huduma kama vile nyumba,umeme
na maji na hivyo basi kuamua kufanya uharibifu.
Lakini visa hivyo vimekosolewa na serikali kwa kuwa waandamanaji huharibu vitu muhimu kama vile shule, maktaba na kliniki.
Mwishowe jamii hizo husalia zikihitaji huduma hizo,serikali inasema.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment