May 25, 2016

Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Riziki Mngwali amehoji Bungeni kwa nini serikali isirudishe mjusi ambaye alichukuliwa mkoani Lindi miaka ya 1900's katika kijiji cha Tandeguru kata ya Mipingo mkoani Lindi na kupelekwa ujerumani ambapo amehifadhiwa.

''Mkoa wa Lindi unaongoza kuwa na rasilimali kubwa tumepiga kelele ya mjusi, mjusi yupo ujerumani wao wanafaidika na mjusi wetu wapanata dola bilioni 3 kila mwaka sisi hatupati kitu''-Amesema Mbunge Riziki.

Mbunge huyo amebainisha kwamba kama mabaki ya mjusi huyo yangerejeshwa kwa kuwa ni kivutio kwa ukubwa wake angeweza kuhifadhiwa kwenye makumbusho nakusaidia ujenzi wa barabara na shule.

Aidha Mbunge huyo amemtaka waziri wa maliasili na utalii aeleze kwa nini tozo inayopatikana huko ujerumani haiwafaidishi wananchi wa eneo husika.

Hata hivyo mjusi huyo mara kadhaa amekuwa akiuliziwa bungeni na serikali kuahidi kulifanyia kazi jambo hilo kwa manufaa ya wananchi.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE