May 20, 2016

Serikali Mwanza imekuta Duka la Madawa linauza Juisi na kiwanda cha Matunda kabisa, walichokifanya?
Mamlaka ya chakula na Dawa TFDA kanda ya ziwa, imelifunga na kulifutia leseni Duka la dawa la Get well Medics lililopo Igoma mkoani Mwanza kwa kukutwa likiuza na kutengeneza juisi badala ya kuuza Madawa Baridi.
Mkaguzi wa TFDA kanda ya ziwa amesema wameamua kulifungia Duka hilo baada ya kukutwa likiuza na kupakia juisi kinyume cha Sheria.
Taarifa Zaidi zinasema kuwa mmiliki wa kiwanda hicho bubu alitumua mbio za haja akihofia kukutana na mkono wa Sheria.
Mkaguzi huyo amekiri kukutwa chupa 470 zilizojazwa juisi aina ya ‘Poa Fruit Drink’ na chupa zingine 300 tupo zikisubiri hatua ya kujazwa kinywaji hicho.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE