May 04, 2016



Picjha 2

Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo leo imetangaza kuisitisha video na wimbo wa Snura, Chura kuchezwa kwenye redio na TV.
Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano wa Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Zawadi Msalla akiongea na waandishi wa habari
Taarifa hiyo imetolewa na wizara hiyo kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wake wa mikutano wizarani hapo jijini Dar. Uamuzi wa kumfungia umekuja kutokana msanii huyo kutojisajili kwenye Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA.

 

“Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja taasisi zake ambazo zinashughulikia mambo ya sanaa, nikimaanisha BASATA, Baraza la Sanaa Taifa, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) pamoja na Bodi ya Filamu, tulipata nafasi ya kukaa pamoja na msanii wa nyimbo za kizazi kipya, Snura Mushi ili tuweze kuangalia kwa pamoja wimbo wake mpya alioutoa hivi karibuni unajulikana kwa jina la Chura, kuangalia maudhui ya huo wimbo na kumuuliza baadhi ya maswali mawili matatu kuhusu kazi hiyo,” alisema Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano wa wizara hiyo, Zawadi Msalla.

                                  

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE