Aliyekuwa meneja wa wasanii walikuwa kwenye kampuni ya Endless Fame
chini ya Wema Sepetu,PetitMan amesema kuwa kwa sasa hayupo tena kwenye
kampuni hiyo kutokana na matatizo ya kifamilia lakini hata tatizo na
Wema Sepetu na kuwa wanaongea kama kawaida.
‘’Endless Fame nilikuwa kama ‘Coordinator’ na pia nilikuwa meneja wa
wasanii, kwa sasa hivi nimesimama kufanya kazi Endless kutokana na
matatizo yetu ya kifamilia na unajua ile kampuni ni kama familia yangu
nimekaa nayo kwa miaka tisa, nimeishi na Wema Sepetu zaidi ya miaka tisa
kwahiyo siwezi kusema kitu chochote kwenye media kwa sababu sina tatizo
na Wema wala Martin Kadinda, matatizo yametokea upande mwingine, kuna
tofauti ilitokea kati yangu mimi na Mirror lakini sasa hivi tuko poa’’
Alisema PetitMan akiwa kwenye kipindi cha Leo Tena.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment