July 06, 2016

Trump 

 Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump amemsifu kiongozi wa zamani wa Iraq Saddam Hussein akisema aliweza kukabiliana vyema na magaidi.
Bw Trump alikuwa akihutubia mkutano wa kampeni eneo jimbo la North Carolina Jumanne alioanza kuzungumza kuhusu kiongozi huyo aliyeuawa kwa kunyongwa Desemba 2006.
“Saddam Hussein alikuwa mbaya, kweli? … Lakini mnafahamu ni jambo gani aliweza kulifanya vyema sana? Aliwaua magaidi. Alifanya hivyo vyema sana,” Trump alisema.
“Hawakuwasomea haki zao, hawakunena lolote. Walikuwa magaidi, mambo yao kwisha.”


Bw Trump awali amewahi kusema kwamba ulimwengu ungelikuwa “asilimia 100 bora kuliko sasa” iwapo viongozi wa kiimla kama Saddam Hussein na kiongozi wa muda mrefu wa Libya Muammar Gaddafi wangelikuwa bado uongozini.
Kabla ya uvamizi ulioongozwa na Marekani, ambapo Saddam aliondolewa madarakani, Iraq ilikuwa imeorodheshwa na Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani kama taifa linalofadhili ugaidi.

  Donald Trump pia aliwahi  kusema kuwa dunia ingekuwa mahala salama zaidi kama tu Saddam Hussein wa Iraq na Maummar Gaddafi wa Libya wangelikuwa hai.

Afisa mkuu mshauri wa Hillary Clinton kuhusu sera, amejibu matamshi ya Bw Trump kwa kusema kuwa: “Sifa za Donald Trump kwa viongozi wa kiimla yamkini hazina mipaka.”
Amesema matamshi kama hayo yanaashiria “ni jinsi gani itakuwa hatari (kuwa na Trump) kuwa Amiri Jeshi Mkuu na jinsi ambavyo hafai kuhudumu kama rais.

Related Posts:

  • New VIDEO | JOZZ D - My Candy Song Name/Jina la Nyimbo: My Candy.Artist Name/Jina la Msanii: JOZZ D .Genre/Aina ya Nyimbo: BONGO FLEVA & AFRO BEATSDirected/Mwongozaji: Remy Ivo Lupamba. Producer/Mtengenezaji: JOHNBGRAND.Studio: GRANDMASTER.C… Read More
  • January Makmba kufunguka jumapilu ijayo   Mbunge wa Bumbuli, Tanga na Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, January Makamba nae ni mmoja wa walioingia kwenye headlines kwamba na yeye ameingia kwenye list ya wagombea wa CCM kwenye nafasi ya U… Read More
  • Idadi ya waliofariki Ghana yafikia 175   Takriban watu 175 wamefariki kufiakia sasa kufuatia moto uliotokea katika kituo kimoja cha mafuta katika mji mkuu wa Ghana Accra. Moto huo uliozuka siku ya jumatano usiku ulianza wakati wakaazi wa mji huo walipok… Read More
  • FIFA:Interpol yataka maafisa 6 kukamatwa  Shirika la maafisa wa polisi wa kimataifa Interpol limetoa ilani ya kukamatwa kwa watu sita wanaohusishwa na FIFA kufuatia madai ya kuhusika na ufisadi. Agizo hilo linawalenga maafisa wanne wa mashirika makuu p… Read More
  • Ulikuwa wapi ya Hussein Machozi  Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu, hatimaye msanii wa bongo fleva Hussein Machozi amekuja na hii hapa mpaya kabisa.  Download hapa chini … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE