Papa
Mtakatifu Benedict XVI alipokuwa akihojiwa alisema kuwa aliona
kujiuzulu kwa ke lilikuwa ni jambo la lazima kutokana na kuporomoka kwa
afya yake na kushindwa kuendana na kasi ya kazi zake.
Japo alitamani kumaliza muda wake wa utumishi, Papa alisema kuwa
alipotembelea Mexico na Cuba Machi, 2012 alijiona kabisa hawezi tena
kuendelea na safari hivyo ni vyema kuachia madaraka.
Alisema kuwa japo alifurahishwa na mapokezi katika nchi ya Mexico na
Cuba, lakini huu ndio wakati alioona kuwa hawezi tena kuendelea
kutekeleza majikumu yake hasa kusafiri safari za kimataifa. Hata
alipotafuta ushauri wa Daktari wake, aliambiwa kuwa asingeweza
kuhudhuria hafla ya Siku ya Vijana iliyofanyika Rio de Janeiro.
Papa alieleza kuwa, licha ya kua alikuwa akiifahamu hali yake, lakini
mwaka 2005 alikubali alipochaguliwa akiamini kua alipaswa kumtumikia
Mungu na kuwa yeye atamuwezesha kufanya kazi.
Papa Benedict XVI alichaguliwa 19 Aprili 2005 kisha akaapishwa
kushika wadhifa huo 24 Aprili 2005 na kujiuzulu nafasi hiyo 28 Februari
2013.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment