Katika kutekeleza hilo wafanyakazi wa NMB nchi nzima wakishirikiana na Kitengo cha Miradi ya Kijamii cha benki hiyo watakuwa wakishirikiana kukusanya pesa kwa ajili ya kutoa msaada.
Jambo hilo litahusisha wafanyakazi kuchangishana pesa wao wenyewe na baada ya kukamilisha mchakato huo, Kitengo cha Miradi ya Kijamii kitakuwa kikiwaongezea pesa sawa na kiwango ambacho walichangishana.
Pia tayari baadhi ya matawi ya NMB nchini yameshaanza kutekeleza mpango huo ambao uewekwa na benki ya kusaidia sehemu ya jamii ambayo inaonekana kuwa na uhitaji.
Baadhi ya matawi yaliyofanya hivyo ni Tawi la NMB Sumbawanga ambalo kwa kushirikiana na Kitengo cha Miradi ya Kijamii walipata 600,000 na kununua mifuko 80 ya saruji na kuwapatia wahanga wa mvua iliyonyesha mjini humo mwezi uliopita kwa ajili ya kufanya matngenezo ya nyumba zao kwa sehemu zilizoharibika.
pic-1  
Meneja tawi la Sumbawanga akimkabidhi Mkuu wa Wilaya Sumbawanga, Dk. Halfan Haule msaada wa mifuko 80 ya saruji. 
pic-2-1 

pic-3-2
Wahanga wa Sumbawanga wakiwa wamepokea mifuko ya saruji kutoka bank ya NMB ikiwa ni maadfhimisho ya wiki ya huduma kwa mteja

pic-4 
Wafanyakazi wa NMB kutoka Idara ya Wateja Binafsi waliwatembelea watoto wa kituo cha Salvation Army kilichopo Kurasini, Dar Es salaam kama sehemu ya kutimiza uwajibikaji wao kwa jamii iliyowazunguka na kuwakabidhi baadhi ya mahitaji maalumu kwa ajili yao.

pic-5 
Wafanyakazi wa NMB Tawi la Kilosa wakiwa na mtoto Sheila (aliyebebwa na meneja wa Tawi Dismas Prosper) ambaye wamemsaidia Milioni 1.4 kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa mguu katika Hospitali ya CCBRT na kupewa mguu wa bandia ambao utamwezesha kutembea na kucheza na wanafunzi wenzake.

pic-6 
Mfanyakazi wa NMB, Victor Rugeiyamu akikabidhi magodoro pamoja na mahitaji mengine ya wanafunzi wa Shule ya Viziwi Buguruni.