June 16, 2017

 

Filamu ya ‘All Eyes On Me’ iliyotengenezwa kwa ajili ya kuonesha maisha halisi ya marehemu Tupac Shakur itaanza rasmi kuonekana leo kwa watu.All Eyes On Me’ iliyozinduliwa jana na hatimaye siku ya leo kupitia kituo cha runinga cha HBO itaanza kuruka, Filamu hiyo ilianza kutengenezwa tangu mwaka jana katika miji mbali mbali ikiwemo Altanta, Sin City na mingineyo nchini Marekani huku ikiwa chini ya mtayarishaji, L.T. Hutton.
Kijana aitwaye Demetrius Shipp Jr. ameigiza katika filamu hiyo kama Tupac huku Danai Gurir akiigiza nafasi ya Afeni Shakur ambaye ni mama mzazi wa rapper huyo ambaye alifariki mwezi Mei, mwaka jana.
 

Tupac alipigwa risasi baada ya kutoka katika  pambano la ndondi kati ya Mike Tyson na Bruce Seldon, Septemba 7, 1996. Na alifariki  dunia Septemba 23 mwaka huobaada ya kupoteza damu nyingi.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE