June 10, 2017

Mwenge wa Uhuru umetembelea miradi mbalimbali Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani  na leo unatarajiwa kumaliza zoezi hilo la kukimbizwa Mkoani humo na kuelekea Mkoa wa Morogoro.
Awali Mwenge huo ulipokelewa na Mkuu wa  Wilaya ya Bagamoyo ,Alhaj Majid Mwanga  ukitokea Kibaha, ambapo katika Wilaya hiyo ya Bagamoyo  uliweza kutembelea miradi yenye thamani ya zaidi ya sh .bilioni 128.
Aidha kwa Halmashauri ya Chalinze Mwenge huo uliweza kutembelea miradi  Tisa  ambapo wamejipanga kuinua uchumi na kupiga maendeleo kupitia viwanda na fursa mbalimbali za kiuzalishaji.
Mwenge huo wa Uhuru uliweza kulala katika Halmashauri hiyo ya Chalinze na unakabidhiwa  Mkoa wa Morogoro leo.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo , Alhaj Majid Mwanga akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka wilaya ya Kibaha, Awali wakati wa Mwenge huo ulipowasili wilayani humo.

Baadhi ya Wananchi wa Halmshauri ya Chalinze wakiwa kwenye mkusanyiko wa Mwenge ambao ulilala hapo kabla ya leo Asubuhi kupelekwa kukabidhiwa Morogoro

Baadhi ya Wananchi wa Halmshauri ya Chalinze wakiwa kwenye mkusanyiko wa Mwenge ambao ulilala hapo kabla ya leo Asubuhi kupelekwa kukabidhiwa Morogoro

Majira ya Asubuhi Mwenge huo ukiendelea na majukumu ya kutembelea miradi mbalimbali katika Halmashauri hiyo  ya Chalinze.

Baadhi ya viongozi na wakimbiza Mwenge wakiwa katika moja ya viwanda katika Halmashauri ya Chalinze wakati Mwenge Uhuru ulipotembelea miradi hiyo leo Juni 10.2017 

Mbunge wa jimbo la Chalinze, Mh. Ridhiwani Kikwete akipata maelezo ndani ya moja ya viwanda ndani ya Halmashauri ya Chalinze wakati Mwenge huo ulipotembelea kukagua miradi mbalimbali.
 

 
Mbunge wa jimbo la Chalinze, Mh. Ridhiwani Kikwete akiwa pamoja na baadhi ya viongozi wa Halmashauri ya Chalinze na Wilaya hiyo ya Bagamoyo wakati wa Mwenge huo ukitembelea miradi mbalimbali kwenye  Halmashauri hiyo. Mwenge huo unatarajia kukabidhiwa Mkoa wa Morogoro leo  Juni 10.2017.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE