September 24, 2017

 Kikosi cha Polisi Moro


 Afisa habari wa timu ya Polisi Tanzania Frank Geofrey akihojiwa na Mwandishi wa habari hizi jana
 
 Afisa habari wa timu ya Polisi Tanizania Afande Geofrey akiwa na Afisa habari wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro Afande Mohamed Ngwaya
 
    TIMU yasoka ya Polisi Morogoro ambaye kwa sasa inajulikana kwa jina la 'Polisi Tanzania' imeamua kuondoka Mkoani Morogoro na kuhamia Moshi Mkoa wa Kilimanjaro. 

Taarifa za kuhama kwa Maafande hao zilizagaa jana kwenye Mjini hapa wakati timu hiyo ilipokuwa wakionyesha kazi na timu ya Mawenzi Market yenye maskani yake Soko la Matunda la Mawezi lililopo kata ya Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro. 

Kufuatia kuzagaa kwa habari hiyo Mwandishi wa Mtandao huu aliamua kumvaa Afisa habari wa timu hiyo Afande  Frank Geofrey ambapo alipotakiwa kuzungumza madai hayo alithibisha kwa kusema.

"Ni kweli timu yetu inahamia Moshi na kuanzia gemu iyajo ambayo tutacheza na Mbeya kwanza tutacheza kwenye uwanja wetu wa nyumba wa Chuo Cha Ushirika Moshi" Alisema Afande huyo Geofrey
 
  Na Dustan Shkidele

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE