September 28, 2017

 

Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniphace Jacob amefunguka na kusema kuwa hawezi kufuta kesi yake dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhusu sakata la vyeti feki na kusema anataka kuona kesi hiyo inafanyika kwa uwazi ili watu wote wajue kinachoendelea
Boniphace Jacob amesema hayo leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari baada ya kutoka kwenye Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na kusema yeye dhamira yake jambo hilo liweze kufika kwenye baraza la maadili ambalo litakuwa ni wazi na watu kusikia na kuona kila jambo ambalo litakuwa likiendelea. 

"Mbaka steji hii hakuna jambo ambalo tumeambiwa limepingwa kwa vielelezo kutokana na jinsi alivyoambiwa ajielezee juu ya vyeti feki, kitu tunachopigania sasa ni kwenda kwenye baraza la mwisho la maadili ambalo ni la wazi ambapo tutamuhoji kwa kila kitu ambacho anatuhumiwa nacho, kwa hiyo kama mimi ndiyo natuhumiwa kwa vyeti nitavitoa hadharani kumuonyesha jaji na watu wote wataruhusiwa kuviona" alisema Meya Boniphace 

Aidha Meya huyo amesema kuwa kitendo cha yeye kuambiwa kuwa amtafute Mkuu wa Mkoa kabla ya jambo hilo halijafika kwenye baraza la maadili anaona jambo hilo limefungua vitisho kwake na mazingira ya ushawishi wa rushwa na kusema hiyo kwake si dhamira yake bali yeye atapenda hilo jambo lifike kwenye baraza la maadili ili kila mtu aweze kufahamu mambo hayo. 
 
"Kitendo cha kumwambia kwamba anitafute tumalizane ili tusifikwe kwenye baraza la maadili binafsi naona limefunguka vitisho na vishawishi ambavyo kimsingi si dhamira yangu mimi nimependa shauri langu toka mwanzo lianze kwa uwazi na liishe kwa uwazi. Kwa hiyo natangazia umma na yeye mwenyewe asikie kuwa mimi dhamira yangu nikiwa hai au nikiwa nimekufa nataka shauri hili lifike kwenye baraza la maadili jambo hili likaendeshwe kwa uwazi na kila mtu ashuhudie" alisema Meya Jacob

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE