Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) Mh. Joseph Mbilinyi amefunguka na kusema ameagizwa na Mbunge
wa Singida Mashariki Tundu Lissu kuwaambia wana Mbeya pamoja na
Watanzania kiujumla kuwa wajiandae.
Joseph Mbilinyi amesema hayo baada ya kumtembelea Tundu Lissu jijini
Nairobi nchini Kenya na kusema kutokana na uimara ambao Tundu Lissu anao
amewataka Watanzania kujianda.
"Nimemtembelea 'Big hommie',
Nairobi hospital. Ameniambia nikawaambie wana Mbeya kuwa alisikia
mwitikio wao wa kishindo nilipomtaja kwenye jukwaa la muziki na kuwa
mwili wake 'uliovunjwa vunjwa' kwa risasi unazidi kuimarika na atasimama
tena. Ameniagiza niwaambie wana Mbeya na Watanzania wote wajiandae,
wajiandae, wajiandae" alisema Sugu.
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini,Mh. Joseph Mbilinyi pamoja na Mbunge wa
Iringa Mjini juzi walimtembelea Tundu Lissu jijini Nairobi Kenya
anapopatiwa matibabu kufuatia kushambuliwa kwa risasi na watu
wasiojulikana akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma Septemba 7, 2017.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment