November 18, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohamed Mahamud ametumia kongamano la Fursa iliyoandaliawa na Clouds Media Group kuomba tamasha kubwa la muziki la Fiesta lifike kisiwani hapo.
Hayo yamebainishwa leo na RC Ayoub katika kongamano la fursa linalofanyika Kisiwani Zanzibar katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi, huku siku ya kesho tarehe 19 mwezi huu likitarajiwa kuhamia katika ukumbi wa Golden Tulip kisiwani humo.
Kupitia mtandao wa kijamii wa Fursa wameandika maneno yanayoashiria Mkuu wa mkoa huyo anahitaji uwepo wa tamasha la muziki la Fiesta lililokuwa likifanyika kwa muda mrefu nchini basi lifike pia katika kisiwa hicho.
Nafahamu ndugu yangu @MutahabaRuge ana nia ya dhati kuinua Zanzibar nimemuomba kwa kua Fiesta nayo ni Fursa naomba ije hapa Zanzibar na amekubali Fiesta itakuja Zanzibar. Mhe. RC Ayoub Mohamed #Zanzibar #AnziaSokoni

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE