December 12, 2017

 Image result for abdulrahman kinana
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Abdulrahman Kinana amefuta mchakato wa kura za maoni za kumtafuta mgombea ubunge kupitia chama hicho katika jimbo la Singida Kaskazini baada ya kugundua kuwa kuna viashiria vya rushwa kwa wagombea wa nafasi hiyo.

Ndg. Kinana amewasimamisha kabisa wagombea wawili, Haider Gulamali na Elia Mlangi kutojihusisha na mchakato huo tena wa kura za maoni na kwa mabadiliko hayo mchakato wa kura za maoni utaanza upya kesho ambapo watu wenye nia ya kugombea watahitajika kuchukua fomu na kujaza kisha kuzirudisha.
Jimbo la Singida Kaskazini limekuwa wazi tangu Mhe. Lazaro Nyalandu ajivue uanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu.
Soma zaidi:


0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE