April 14, 2018

 
Mona akiwa na mpinzani wake Lupita Nyongo toka Kenya
 
Mrembo na muigizaji mkongwe kwenye tasnia ya filamu nchini Yvonne Cherrie maarufu kama 'Monalisa'  ameibuka mshindi kwenye tuzo za 'The African Prestigious Awards' nchini Ghana akimbwaga mpinzani wake Lupita Nyong'o.
Katika tuzo hizo zilizotolewa usiku wa kuamkia leo huko jijini Accra nchini Ghana Monalisa ametwaa tuzo katika kipengele cha 'Best African Actress'. Kwa mujibu wa tuzo hizo Monalisa sasa ndiye muigizaji bora wa kike barani Africa.


Monalisa amethibitisha ushindi wake kupitia mtandao wa 'Instagram' ambapo amepandisha picha akiwa na tuzo yake na kuandika ujumbe huu  

''Tumeshindaaaaaaa narudi home na Tuzo za kutosha.Ahsante Watanzania,Nawapenda mno''.
 
Kwa ujumbe huo wa Monalisa unaashilia huenda pia kuna tuzo nyingine wameshinda Watanzania ambao walikuwa wanawania vipengele mbalimbali katika tuzo hizo kubwa za filamu nchini Ghana.
Watanzania wengine waliokuwa wanawania ni King Majuto kipengele cha Mchekeshaji Bora Afrika, Vicent Kigosi kipengele cha msanii Bora wa Kiume Afrika na Mpiga picha Mahiri Moiz Hussein katika kipengele cha Mpiga Picha Bora Afrika.

Related Posts:

  • Never Forget Moro - Hoodbangerz Kufuatia tukio la ajali ya Moto uliosababishwa na Roli la Mafuta na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 75 mkoani Morogoro, tukio lililotokea 10 August 2019 siku ya Jumamosi katika eneo la Msamvu, wasanii wa Hood Bangerz … Read More
  • BBC Dira ya Dunia leo hii 19 june 2019   Ifuatayo ni dira ya Dunia ya BBC inayokutangazia toka jijini London uingereza. Taarifa ya habari usiku wa leo 19 june 2019. Msomaji wako ni Zuhra Yunus           … Read More
  • Vanessa Mdee kuiwakilisha Tanzania kwenye meza ya majaji   Msanii muziki wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee ataiwakilisha Tanzania kwenye meza ya majaji wanne waliotangazwa na waandaaji wa shindano la East Africa’s Got Talent 2019. Majaji wengine watatu waliotangazwa jana wa… Read More
  • Brand New Song: Zombie President - R I P Ngwair   Mwanamuziki na Mtangazaji Maarufu kutoka mkoani Morogoro MC Calvin Maarufu Zombie President, ameachia wimbo wake mpya kabisa uitwao R I P Ngwair. Wimbo wa R I P Ngwair ni wimbo unaoonesha mapenzi ya wazi kabisa k… Read More
  • Huawei wapigwa stop Facebook Kampuni ya Facebook imeingia rasmi katika vita vya kiuchumi baina ya Marekani na China ikizuia huduma wezeshi (APP) zake kutumika katika simu za Huawei. Zuio hilo linalenga huduma mama ya Facebook na nyingine kutoka … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE