April 12, 2012


Berry Black akipagawisha jukwaani

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya Mbaraka Abdallah anatarajia kutambulisha wimbo wake mpya uitwao Nyumbani Sio Safi, Jumapili kwenye Ukumbi wa Club Billicanas.

Berry amesema katika onyesho hilo maalumu kwa ajili ya utambulisho wa wimbo wake, ataambatana na msanii mwenzake Isihaq Salehe ‘Easy Man’, anayeng’ara na kibao cha Kasoro Wewe.

“Katika onyesho hilo la Jumapili nitatambulisha wimbo wangu huo lakini pia nitakuwa na nyingine kibao za kuwapagawisha mashabiki wangu, nikisindikizwa na swahiba wangu Easy Man,” alsiema Berry Black.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE