October 12, 2012

  

Msanii wa hit ya ‘Mkono Mmoja’ Chege Chigunda aka Mtoto wa Mama Said ametupiwa shutuma kali kuwa amemzalisha mke wa mtu.

Akiongea na U Heard ya Clouds FM leo, mume huyo aliyejitaja kwa jina la Jose mkazi wa Kasulu mkoani Kigoma amesema mke wake aitwaye Salma amejifungua mtoto anayefanana kila kitu na Chege.



Akizungumza kwa jazba, Jose amesema yuko tayari kwenda kuchukua vipimo vya DNA na kama vikionekana negative atamlipa Chege shilingi milioni tano.

Amesema kesho anaanza safari yake ya kuja Dar es Salaam kumleta Salma na mwanae kwa Chege ambaye anasema ndiye baba yake mzazi huku akitishia kumfanyiaa kitu mbaya staa huyo.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Chege aliyekuwa akiongea kwa dharau amesema hajui lolote na wala hamfahamu Salma.



Kwa   upande  mwingine  wadau  wemesema  kwamba  inawezekana  ni  story  ya  uwongo  CHEGE  labda  ametengeneza  kwani  wasanii  wengi  sasa  hivi  huwa  wanajitungia  skendo  ili  wapate  kuzungumzwa  hasa  wanapiokuwa  na  nyimbo  mpya  au  wanapokaribia  kutoa  nyimbo  mpya.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE