November 30, 2012


                                                                   Shalo milionea  enzi  za  uhai  wake


Watu wanne wamekamatwa na Jeshi la Police kwa tuhuma za na kumuibia marehemu Sharo Milionea baada ya kupata ajali ya gari na kupoteza maisha.

Kwa mujibu wa website ya thisisdiamond.com watu hao wamekutwa na vitu alivyokuwa navyo marehemu Sharo Milionea kama vile
T-shirt, Viatu, Simu ya mkononi, Pete, Cheni, Tairi moja la gari , pamoja na Battery la gari ambalo marehemu alipata nalo ajali.

Taarifa za awali zinasema watuhumiwa hao walikuwa sita lakini wamekamatwa wanne hadi sasa, na jeshi la Polisi linaendelea kuwasaka watuhumiwa wawili.

Inasemekana watu hao waliamua kumkata vidole marehemu baada ya kushindwa kumvua pete.
Hata hivyo jeshi la polisi bado halijatoa taarifa rasmi kuhusiana na kukamatwa kwa watu hao.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE