May 13, 2013

                  Mfalme  Sele  akiwa  na  MSANII  MWENZAKE  Tall  Balle  Ballet  Wallet

    Msanii  wa  muziki  wa  Hip  Hop  toka  mkoani  Morogoro  mwenye  taji  la  ufalme,  afande  Sele  amesema  lengo  la kuandika wimbo  wa  Dini  Tumeletewa  ni  kutaka  kumrudisha  mwafrika  katika  tamaduni  zake.  Katika ukurasa  wake  wa  Facebook  Afande  amepost.  Katika wimbo  huwo  ambao  Mbunge  wa  Kigoma  Kaskazini  Kabwe  Zuberi  Zitto  amehaidi  kuufanyia  Video  kwa  pesa  yake,  Afande  amejaribu  kuzungumzia  amani,  imani  na  mila  kuhusiana  na  kuabudu.
 
    ''Lengo la hii kazi yangu mpya DINI TUMELETEWA ni kumrudisha mwafrika kwenye uafrika wake ambao msingi wake ni UMOJA, USHIRIKIANO NA UPENDO. Ambao kwa siku za hivi karibuni tumeshuhudia ukitoweka. Tumeona mapigano/mauaji ya itikadi za kidini wenyewe kwa wenyewe, pia kuelezea uhuru wa kuabudu kwa imani yoyote bila kuvunja sheria za Taifa letu. Kwa mtu yoyote makini mwenye mapenzi mema kwa Taifa letu na AFRIKA hawezi kupingana na hilo, kwa kutambua hilo MH; ZITTO ZUBERI KABWE(ZZK) kajitolea kugharamia gharama zote kwa ajili ya kufanikisha vidio bora kabisa ya wimbo huu, hii ni kazi yetu wote mimi na wewe, tunasema asante sana kwa Mh; Zitto. AMANI NA UPENDO KWANZA''

Team amani na upendo follow me twitter @afandeseleking.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE