January 23, 2014

Nay
  Mkali wa Hip Hop Tanzania anyemiliki tuzo moja ya wimbo bora wa Hip Hop 2012 - 2013  Nay wa mitego, ameweka wazi zamila yake ya kumuunga mkono Waziri mkuu mstafu Edward Lowasa.
 Akizungumza  leo Nay wa Mitego amesema baada ya kumuimba Lowassa katika wimbo wake Salamu Zao, amepokea maoni kutoka kwa vijana kuwa Lowassa ndiye kiongozi atakayeifaa Tanzania.
“Nikizungumzia kuhusu Lowassa yaani kila mtu anam-support,kwasababu hata ukiangalia comment za kwenye Instagram kila mtu anamadmire. Mimi sio mwanasiasa na wala siwezi siasa lakini ni mtu ambae namkubali sana .Mimi namkubali sana na kama ikiwezekana tukatuma maombi pia awepo kwenye wagombea Urais wa 2015,sijui kama yeye yupo na plan hiyo lakini vijana na mimi tumetokea kumwelewa sana na nimegundua watu wengi wapo nyuma yangu,”amesema Nay wa Mitego

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE