February 15, 2014

Kamishna Mkuu wa Uhamiaji anatangaza nafasi za kazi katika Idara ya Uhamiaji. Nafasi hizo ni Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Koplo wa Uhamiaji na Konstebo wa Uhamiaji.
A.MKAGUZI MSAIDIZI WA UHAMIAJI (Nafasi 70)
SIFA ZINAZOHITAJIKA
-Awe na Shahada ya Kwanza au Stashahada ya Juu kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa  na Serikali katika fani zifuatazo:
Sheria, Uchumi, Biashara, Utawala, Uandishi wa Habari, Ualimu, Usafirishaji, Raslimali Watu, Sayansi ya Kompyuta, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Takwimu, Uchapaji, Uhandisi Majengo na Uhandisi Mitambo.
-Awe na umri usiozidi miaka 35
MAJUKUMU NA KAZI ZA KUFANYA
-Kusimamia doria sehemu za Mipakani, Bandarini, Vituo vya Mabasi, Treni na sehemu zenye vipenyo vya kuingia na kutoka nchini vikiwemo vya majini
-Kusimamia shughuli za upelelezi, kuandaa Hati ya Mashitaka na kuendesha mashitaka
-Kutoa na kupokea fomu mbali mbali za maombi ya Hati za Uhamiaji
-Kufanya Ukaguzi wa Mwanzo wa Maombi mbalimbali
-Kuagiza ufunguaji wa Majalada ya watumiaji
-Kupokea na kukagua Hati za Safari, Fomu za Kuingia na Kutoka Nchini
-Kuidhinisha malipo mbalimbali ya huduma za Uhamiaji kwa wanaostahili
-Kutunza kumbukumbu za ruhusa za watu wanaoingia na kutoka nchini
-Kukusanya, kusimamia na kutunza takwimu za Uhamiaji na Uraia
-Kuandaa majibu ya maombi yote ya huduma za uhamiaji yaliyokubaliwa au kukataliwa

                    Zaidi ingia: ajirazetu.com

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE