Kampeni ya Ng’arisha Tanzania inahamasisha kuweka mazingira ya jiji katika hali ya usafi na kupendeza na pia kutunza mazingira,Kampeni hii itahusisha kufagia baadhi ya mitaa katika manispaa ya Ilala,kuzoa taka na kuzitupa maeneo husika au kuziteketeza.
Kutokana na hayo Rose Ndauka kama msanii wa filamu na akiwa kama kioo cha jamii ameamua kuwashirikisha viongozi,raia wa kada mbalimbali na mamlaka husika kuendesha kampeni hii ya Ng’arisha Tanzania siku ya Jumamosi tarehe 15 Machi 2014,kuanzia saa moja asubuhi hadi saa 5 asubuhi.
Wasanii wenzake waliothibitisha kuwepo kwenye kampeni hiyo mpaka sasa ni pamoja na Monalisa,Yusuph Mlela,Slim Omary,Riyamma Ally na wengine wengi.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment