March 14, 2014

10 
Msanii kutoka kiwanda cha filamu Tanzania Rose Ndauka amekuja na kampeni ya usafi maalun kwa ajili ya kuliweka safi jiji la Dar es salaam na wilaya zake ambayo ameipa jina la Ng’arisha Tanzania ambayo anategemea kuianza Jumamosi ya March 15.
Kampeni ya Ng’arisha Tanzania inahamasisha kuweka mazingira ya jiji katika hali ya usafi na kupendeza na pia kutunza mazingira,Kampeni hii itahusisha kufagia baadhi ya mitaa katika manispaa ya Ilala,kuzoa taka na kuzitupa maeneo husika au kuziteketeza.
6 
Kwa kuwa jukumu la usafi katika miji linafanywa na mamlaka husika lakini pia kufanya usafi ni jukumu la kila raia hasa katika maeneo tunayoishi na kufanyia shughuli zetu za maisha pia ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa hatuwi chanzo cha kuweka miji katika hali chafu.
Kutokana na hayo Rose Ndauka kama msanii wa filamu na akiwa kama  kioo cha jamii ameamua kuwashirikisha viongozi,raia wa kada mbalimbali na mamlaka husika kuendesha kampeni hii ya Ng’arisha Tanzania siku ya Jumamosi tarehe 15 Machi 2014,kuanzia saa moja asubuhi hadi saa 5 asubuhi.
Wasanii wenzake waliothibitisha kuwepo kwenye kampeni hiyo mpaka sasa ni pamoja na Monalisa,Yusuph Mlela,Slim Omary,Riyamma Ally na wengine wengi.

Related Posts:

  • Umeipata hii ya majaji 3 kufutwa kazi kwa kutazama video za ngonoMajaji watatu wamefutwMajaji watatu wamefutwa kazi kwa kutumia muda wao afisini kutizama filamu za ngono. Jaji Timothy Bowles anayesikiza kesi za wilaya , jaji wa maswala ya uhamiaji Warren Grant na jaji Peter Bullock wamefut… Read More
  • Makamu wa rais wa afutwa kazi    Rais wa Sierra Leone Ernest Bai Koroma amemfuta kazi makamu wa rais kwa kutafuta hifadhi katika ubalozi wa kigeni nchini humo.Siku ya jumamosi ,Samuel Sam Sumana amesema kuwa alimtaka balozi wa Marekani kump… Read More
  • Gari la kikosi cha Zimamoto limevunjwa vioo   Picha hii siyo halisi ya tukio   Jeshi la Polisi mjini Tunduma mkoani Mbeya limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya vijana waliofunga barabara. Akiongea na East Africa Radio kwa njia ya simu Kaman… Read More
  • Fid Q, K-sha wapata tuzo zaheshima za EU    Kutoka kulia ni baadhi ya Watanzania waliotunukiwa Tuzo ya Heshima na Umoja wa Ulaya nchini EU, kutokana na mchango wao katika kuliletea taifa maendeleo.   Umoja wa Ulaya nchini umewatunuku tuzo za hes… Read More
  • Kenya yapunguza safari zake Tanzania   Shirika la ndege la Kenya, Kenya Airways leo limeanza rasmi kupunguza safiri zake katika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam kufuatia agizo la mamlaka ya anga ya Tanzania kuamuru shirika hilo kupunguza safari zake k… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE