April 24, 2014

 
 Afisa wa polisi akilinda mojawapo ya maeneo katika jiji la Nairobi ambalo usalama wake unatatiza.

Watu wanne, wakiwemo maafisa wawili wa polisi, wameuawa jana usiku mjini Nairobi baada ya gari walilolizuia kulipuka, lilipokuwa likielekea katika kituo cha polisi katika eneo la Pangani, jijini Nairobi.
Bomu la pili lilipatikana katika gari hilo baada ya mlipuko huo na wataalamu wa mabomu waliliharibu.
Maafisa wa polisi wanasema wanajaribu kuitambua miili ya washukiwa hao ambayo iliharibiwa vibaya kiasi cha kutoweza kutambulika.
Usalama umeimarishwa katika eneo hilo na polisi wanaendelea kufanya uchunguzi.
Bosco Mugendi ana kibanda cha kuuza vitu vidogovidogo karibu na lango la kuingia kwenye kituo cha polisi cha Pangani kulikotokea mlipuko huo.
Alunukuliwa akisema:"kile kilichonikuta katika kibanda changu ni nyama ya watu iliyonirukia halafu mimi nikatoroka na kutoka nje."
Mtaalamu wa maswala ya usalama jijini Nairobi, George Musamali, aliambia BBC kuwa maafisa wa polisi waliokuwa wakisindikiza gari kuelekea kituo hicho cha polisi walikuwa kwenye gari la washukiwa

Related Posts:

  • Rais Kikwete ajivunia kuwabeba wanawakeRais Jakaya Mrisho Kikwete amesema anajivunia kuona anamaliza muda wake akiwa amefanikisha kujenga msingi imara ya kuwawezesha na kuwapa nafasi wanawake katika ngazi za uongozi na hivyo kuwataka viongozi wajao waendelee kuwap… Read More
  • Chinja chinja wa IS alikuwa mlevi   Mohammed Emwazi ,mtu ambaye alibadilika na kuwa ''chinja chinja'' wa kundi la islamic state kwa jina 'jihad John' Mohammed Emwazi, alifurushwa kutoka nchini Tanzania kwa kuwa mlevi na mtu anayetoa matusi.,afisa m… Read More
  • Ubunge Morogoro Mjini, hatimaye Maharagande avaa gwanda rasmi   Maharagande akipokea fomu za kuwania nafasi ya kuteuliwa kuwa mgombea wa ubunge morogoro mjini kutoka kwa katibu kata ya Sultani Area Amin Kabwanga katikati, wanaoshuhudia tukio hilo kushoto ni M/kiti CUF  Moro… Read More
  • Mtatiro: Nitagombea Ubunge Segerea   Ndugu zangu, kesho Jumatatu 09 Machi 2015 saa 4.00 asubuhi, nitachukua fomu ya kuwania ubunge katika jimbo la Segerea kama ambavyo taratibu za ndani ya chama changu zinaruhusu. Hakutakuwa na mbwembwe vifijo wala … Read More
  • Wanawake waombwa msamaha wanawake wakifanya maandamano kuadhimisha siku ya wanawake duniani nchini Indonesia   Kampuni inayotengeneza nguo za riadha nchini Indonesia, imeomba msamaha, kwa kuuza t-shat… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE