Binti Fauzia akiwa amepozi nyumbani kwao maeneo ya Kigogo jijini Dar es Salaam
NI lipi hujasikia? Linaweza kuwa hili! Binti mmoja aliyetambulishwa
kwa jina la Fauzia (jina la mbele lipo), mwenye umri wa miaka 16, mkazi
wa Kigogo jijini Dar amedai kutumikia nafasi ya umalkia katika imani
yenye utata duniani ya Freemason, Uwazi linakudondoshea.
Binti huyo alikwenda mbele zaidi kwa kudai kwamba ili kujiunga na imani hiyo, alimuua mama yake mdogo kwa ajili ya kafara.
Akizungumza na gazeti hili siku chache baada ya kuokoka akiwa
nyumbani kwa baba yake mdogo, Kigogo, Fauzia alisema alitokea Wilaya ya
Kahama mkoani Shinyanga alipokuwa akiishi na bibi yake.
Alikuja Dar kwa lengo la kuendeleza mauaji ya kafara ambapo safari hii ilikuwa amuue mama yake mdogo mwingine ambaye ni mjamzito kwa sasa.
Alisema kama angefanikiwa kumuua, angepandishwa cheo na kuwa malkia kamili katika jamii hiyo inayotafsiriwa vibaya duniani.
Alikuja Dar kwa lengo la kuendeleza mauaji ya kafara ambapo safari hii ilikuwa amuue mama yake mdogo mwingine ambaye ni mjamzito kwa sasa.
Alisema kama angefanikiwa kumuua, angepandishwa cheo na kuwa malkia kamili katika jamii hiyo inayotafsiriwa vibaya duniani.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment