
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi
ameanza kampeni kanisani kuwataka wananchi kupinga serikali tatu
zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, vinginevyo nchi
itatawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano itashindwa kuwalipa
mishahara wanajeshi.
Alisema hayo jana katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Katika
hotuba yake, Lukuvi aliwaeleza waumini waliofurika katika ibada ya
kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa askofu wa kanisa hilo katika
jimbo kuwa waendelee kuliombea Bunge lifanye uamuzi sahihi wa serikali
mbili.
Aliwataka Watanzania kuipuuza Rasimu ya Katiba katika suala la Muungano na Serikali tatu kwa madai kuwa kutaka kuwapo mfumo huo ni kutaka Watanzania waingie vitani.
Aliwataka Watanzania kuipuuza Rasimu ya Katiba katika suala la Muungano na Serikali tatu kwa madai kuwa kutaka kuwapo mfumo huo ni kutaka Watanzania waingie vitani.
“Serikali
tatu zikipita ni wazi kuwa hata makanisa yatafungwa kwani nchi haiwezi
kuwa na amani tena, angalieni nchi ya Korea Kusini na Korea Kaskazini
ambao waligawanyika na sasa ni maadui wakubwa wanaokaa mipakani
wamenyoosheana bunduki,” alisema na kuongeza:
“Waumini ndugu zangu wapendwa, kwa sasa tupo katika hali mbaya sana hapo bungeni, tunaomba mtuombee kuna watu ambao wanataka madaraka kwa nguvu na wameanza kutafuta jinsi ya kuvunja Muungano na kudai kuwapo kwa Serikali tatu, nawaomba sana wapuuzeni wale wote ambao wanataka serikali tatu.”
“Waumini ndugu zangu wapendwa, kwa sasa tupo katika hali mbaya sana hapo bungeni, tunaomba mtuombee kuna watu ambao wanataka madaraka kwa nguvu na wameanza kutafuta jinsi ya kuvunja Muungano na kudai kuwapo kwa Serikali tatu, nawaomba sana wapuuzeni wale wote ambao wanataka serikali tatu.”
Source:MATUKIO NA VIJANA
0 MAONI YAKO:
Post a Comment